Acha kulalamika kuhusu kazi yako na fanya mambo haya mawili.

Acha kulalamika kuhusu kazi yako na fanya mambo haya mawili.

Ndugu msomaj habari za siku ya leo. Nakukaribisha katika makala ya leo.
Ajira kwa sasa ni changamoto kubwa sana hasa hasa kwa vijana na pia katika nchi zinazoendelea hasa dunia ya tatu. Si tu katika kuipata bali pia katika kuifanya.
Labda nianze kwa kukueleza kuwa tangu nikiwa mwanafunzi mpaka sasa nimebahatika kukutana na wafanyakazi wengi ambao wamekuwa wakilalamika kuhusu kazi zao, nazungumzia katika kada nyingi nilizobahatika kukutana nazo hasa wafanyakazi wa ngazi ya chini na kati. Kila mtu analalamika kuhusu kitu ambacho yeye anakikosa anatendewa. Lakini wengi wamekuwa wakilalamika kuhusu maslahi duni (mishahara na marupurupu), mazingira magumu ya kazi, manyanyaso kutoka kwa wakubwa wao wa kazi, kudharaulika, kupuuzwa na hata kutokusikilizwa na mengine yanayofanana na haya.

Mbali na kwamba tatizo linaweza kuwa kwa wanaolalamikiwa kwa kutotekeleza majukumu yao pia kuna wafanyakazi wasiotekeleza majukumu yao. Hilo tatizo pia tatizo kubwa ni kwamba wafanyakazi wengi wamekuwa watu wa kulalamika bila kuchukua hatua. Unakuta mtu kaajiriwa mwanzoni mwa miaka ya tisini bado analalamika kuhusu hali aliyoikuta bila yeye kashindwa kuibadili au yeye mwenyewe kubadillika. Kulalamika na kulaumu kamwe hakuwezi kutatua tatizo lako kazini bali kuchukua hatua pekee ndio njia ambayo inaweza kusaidia. Kuna hatua kadhaa ambazo utatahitaji kuchukua kama mfanyakazi ambaye unaona hautendewi inavyopasa.

Hatua ya kwanza ni kubadili mtazamo kuhusu kazi unayoifanya. Jitathmini na kuweza kugundua wapi kuna tatizo kati yako na mwajiri wako. Yawezekana kuna matatizo kidogi kwenye ajira yako kulinganisha na wewe unavyochukulia. Mapungufu hayawezi kukosekana popote hivyo mengine yapasa uyazoee na kuchukulia kama sehemu ya changamoto za kazi. Matatizo mengi yanaanza kwenye mtazamo wako (attitude) kuhusu jambo fulani. Kama ukijenga mtazamo hasi basi utaona kila kitu ni kibaya lakini ukiojenga mtazamo chanya utaona mazuri kuliko mabaya. Kama pia wewe ni muoga kuchukua hatua ambayo nitaitaja hapa chini basi bora ukubaliane na kazi yako na kuamua kuifanya kwa moyo wako. Wengine ni waoga sana kuchukua hatua hiyo, huwaza wataishije. Jipime na uangalie kama unaweza kubadili kitu kibadili na kama huwezi kubadili kubaliana na hali halisi iliyopo.

 Kubadili kazi yako kwa kufanya kazi nyingine. Ndugu yangu hii ni hatua ngumu sana kwa watu walio wengi hasa ambao wamekaa kwenye ajira kwa muda mrefu na pia wana majukumu mengi. Najua ilivyo ngumu sana kuacha kazi ambayo ndiyo ilikuwa kila kitu kwako lakini kama haikupi yale ambayo ulikuwa ukiyapata kabla huna budi kujikaza na kuchukua hatua hii. Mwanafizikia maarufu zaidi wa karne ya 20 aliwahi kusema kwama kuendelea kufanya kitu kile kile kwa namna ile na kutegemea matokeo tofauti ni ujinga. Kwa mfano umekuwa ukilipwa hela ndogo sana kiasi kwamba huwezi hata kujiwekea akiba ama hautoshelezi kiasi kwamba unaweza kuwa unaishi kwa madeni tu na wakati huo ukitegemea kufanikiwa katika kujiletea maendeleo utakuwa ni zaidi ya muujiza. Sisemi kwamba wote wanaoshindwa kujiwekea akiba kunatokana na kulipwa hela ndogo, la hasha kuna wengine wanshindwa kujiwekea akiba kutokana na matumizi yao mabovu ya hela. Ila kuna wengine kweli ni ngumu kujiwekea akiba kwa vipato vyao vidogo na majukumu mengi. Suluhisho hapo ni kutafuta kazi nyingine unayoipenda kabla hujaacha uliyonayo ama kuanza kufanya shughuli nyingine tofauti na ajira yako yaani kujiajiri au ujasiriamali. Pia kuna mtu aliwahi kusema Kama kile unachofanya hakikupi tena faida ni bora kukiacha. Kunahitaji ujasiri mkubwa sana kwa baadhi ya watu kuacha kazi. lakini kabla hujaogopa kuacha kazi, jaribu kujiuliza itakuwaje siku ukifukuzwa kazi? Je utaishije, je utakufa? naomba ujijibu mwenyewe. Tatizo la wafanyakazi wengi ninkwamba hawajiandai kustaafu tokea siku ya kwanza ya ajira. Kumbuka huna uhakika na ajira yako maana huhusiani moja kwa moja na mwajiri wako kiasi kwamba utafanya kazi hiyo mpaka ufikie umri wa kustaafu kwa lazima. Hivyo basi ni muhimu kujipanga kabla hujapangwa. Ni bora kabisa uanze kutafuta vyanzo vingine vya mapato kwa kujiajiri, kufanya biashara au ujasiriamali wakati ukiendelea na kazi unayoifanya ili ikitokea umeacha basi uwe na pa kuanzia.
Soma: Je umepanda nini shambani kwako?

Wengine huogopa kuacha kazi kwa sababu hawana akiba yoyote waliyojiwekea. Yaani maisha yake ni kula tu yaani anafanya kazi aishi, waingereza husema Living hand to mouth. Ndugu yangu ukiishi hivyo ujue kwamba hakika utakufa masikini. Sikutabirii ila ndio ukweli wenyewe huo. Mtu mmoja aliwahi kuniambia usiishi kama mvuvi (samahani wavuvi), kwani wavuvi walio wengi hawaamini katika kujiwekea akiba maana anajua ziwa, mto ama bahari wanakovua zipo milele na atavua tu. Tabia hii huwafanya watumie mapato yao vibaya na kushindwa kujisaidia wakati ambapo hawana nguvu, wagonjwa, wamezeeka ama hakuna tena samaki kwa kipindi fulani au serikali kusitisha uvuvi ili kuruhusu samaki kuzaliana.

Nipende kuhitimisha tu kwa kukuambia kuwa kuendelea kulaumu, kunung´unika ama kulalamika hakutasaidia kama wewe hujaamua kutafuta suluhisho. Kumbuka kwamba maisha ni yako na mfanya maamuzi ni wewe. Ukiamua kuendelea kulia ni sawa pia na ukiamua kuchukua hatua ni bora zaidi. Changamoto ni sehemu ya maisha na uchaguzi ni wako uishije, mfano unaweza kuhainga sasa hivi ukaishi vizuri kesho ama uishi kwa starehe leo ukahangaike kesho.
Nyakati ngumu hazidumu lakini watu wagumu hudumu (Tough times never last but tough people do),nimenukuu kutoka kwa mwandishi Robert H.Schuller.
Nakutakia siku njema, kwaheri.

Nickson Yohanes
Email: nmyohanes@gmail.com

Ili uweze kupata mafanikio ni lazima ulipe gharama hizi

Habari za muda huu ndugu msomaji wa mtandao huu wa PAMBAZUKA DAIMA, natumaini kuwa hujambo na unaendelea vyema na harakati za kujiletea maendeleo , kama hauko vyema basi pole na kumbuka kuwa hizo ni changamoto za maisha ambazo tunazipitia.

Je unalipa gharama za mafanikio?
Hili ndilo swali ambalo unatakiwa kujiuliza kabla hujaendelea mbele, kisha fuatana nami hapa chini ili tusome kwa pamoja.
Neno mafanikio ni neno linalovutia sana kulisikia masikioni, najua kwanini ni kwa sababu kila mtu ananyatamani na kuwaza kuyafikia mafanikio. Kuna mafanikio yapo katika nyanja zote kama afya, elimu, fedha na hata kiroho. Mafanikio huja kwa njia nyingi na namna mbali mbali lakini kuna kanuni kubwa ya kuweza kufanikiwa. Kanuni hiyo ni kulipa ghara za kufanikiwa. Hakuna yeyote alieyewahi kufanikiwa bila kulipa gharama zinazotakiwa kuweza kufanikiwa. Kama unataka kufanikiwa basi kuwa tayari kulipa gharama hizo. Wengi hujaribu kukwepa kulipa gharama na kuamua kutumia njia ya mkatio ya kutafuta mafanikio. Ukweli ni kwamba hakuna njia ya mkato bila kulipa gharama, na mara nyingi ukijaribu kukwepa gharama utajikuta unalipa gharama kubwa sana baadae.


Miongoni mwa gharama za kulipa ni muda wako. Ni lazima uwekeze muda wako katika kile ambacho unakifanya. Kwa mfano kwa mwanafunzi itamlazimu yeye kuutumia muda wake mwiingi kwa kusoma na kujiandaa na mitihani na kwa upande wa mkulima atautumia muda wake mwingi kuhudumia shamba lake. Lazima uutenge muda wa kutosha kwa shughuli ama jambo lile ambalo umepanga kulifanikisha. Tumia muda wako vizuri maana huwezi kuulinda muda bali unaweza kuutumia vyema, kumbuka tu kwamba kila mtu ana saa 24 tu na hakuna mwenye zaidi ya hapo. Matumizi mazuri ya muda wako kwa kuwekeza katika kile cha kuweza kukuletea mafanikio ndiyo yatayokutofautisha wewe na wale ambao hawajafanikiwa. Usiutumie muda wako katika vile vitu ambavyo si muhimu na havikusaidii kusonga mbele kuelekea kwenye mafanikio kama muda mwingi wa kupiga soga, kutumia muda mwingi katika mitandao ya kijamii na kuzurura.

Gharama ya kufanya kazi kwa juhudi na maarifa, huu ni ukweli ambao lazima sote tuujue. Huwezi kufanikiwa kama hufanyi kazi, tena ufanye kazi kwa juhudi na maarifa. Sio nguvu peke yake bali maarifa pia lazima yawepo maana kuna watu wengi sana ambai ni hodari wa kufanya kazi lakini ni masikini wa kutupwa. Lazima ujue ni wapi hasa pa kuwekeza juhudi zako. Mbali na hilo ni lazima pia ujiongezee maarifa kupitia njia mbalimbali mfano kusoma sana vitabu. Maarifa mengi tuyatakayo yapo kwenye vitabu, yameshaandikwa tayari. Pia kuhudhuria semina na matamasha yanayokuongezea maarifa katika kile unachofanya. Kwa mfano wewe ni mfanyabiashara unaweza kuhudhuria semina za kukuza mitaji, uwekezaji na hata mauzo.

Uvumilivu ni gharama nyingine ambayo unatakiwa kuilipa. Kama ukitaka kufanikiwa kweli ni lazima uweze kulipa gharama hii. Uwezo wa kuweza kuvumilia ndio utofauti wa kipekee uliopo miongoni mwa waliofanikiwa na wasiofanikiwa. Watu wengi wenye kuvumilia kuyasubiri mafanikio huku wakiendelea kujituma ni dhahari kuwa watafanikiwa. Usiwe na tamaa ya kupanda na kuvuna kesho, Mfikirie mkulima wa miti ambae hupanda miti na kusubiri zaidi ya miaka minane, kama sio mvumilivu asingeweza kuipanda miti hiyo. Kuna dhoruba nyingi kufika huko lakini huna budi kuvumilia kama kukatishwa tamaa, kuanguka na kadhalika lakini huna budi kufika kileleni. Kumbuka tena hakuna njia rahisi wala ya mkato ya kuyafikia mafanikio isipokuwa kwa kuilipa gharama. Jiwekee lengo kwamba utafanikiwa na lazima utafanikiwa tu.

Gharama za fedha, fedha ni muhimu sana tena sana. Pesa ni mtumishi mwema sana ambaye anaweza kukufanyia kazi zako na kukuletea faida. Hakuna mtu hata mmoja ambaye anasema pesa sio muhimu. Utahitaji fedha ili uweze kuwekeza, kufanyia biashara, kuisha na mengine mengi ambayo unayajua kuhusu fedha. Kuwa tayari kulipa gharama za kifedha kuweza kufanikiwa. Wekeza pesa ili uweze kufanikiwa ili uweze kupata faida pia.

Kujitoa sadaka (self-sacrifice), Hili ni la lazima sana kuweza kufanikiwa. Hakuna njia nyingine ndugu lazima ujiotoe sadaka, lazima ukubali kuyasotea mafanikio yako. Mwanzoni mambo huwa magumu sana hata kukufanya ukate tamaa. Uvumilivu na imani kubwa ni muhimu sana kwa kipindi hiki. Bondia maarufu sana dunia marehemu Muhammad Ali aliwahi kusema ``Niliichukia kila dakika ya mafunzo lakini nikasema ´Usiondoke´Teseka sasa ili uishi maisha yako yote kama mshindi´´. Ni lazima ujitoe kweli kweli, ni lazima uamue kutafuta kile unachokitaka. Mafanikio sio rahisi ndio maana sio watu wengi wamefanikwa. Ni lazima uamke mapema, ni lazima ufanye kazi hata kama hupendi, lazima kujifunza, lazima uchelewe kulala wakati mwingine, kujinyima baadhi ya vitu, kutokubali kukatishwa tamaa na vingi vingine.

Upendo nao ni gharama nyingine ya kulipa, unaweza kuiona ndogo lakini si kweli. Utahitajika kuwapenda maadui zako, wabaya wako, washindani wako na hata washindani wako. Utahitaji kuwapenda watu ili ujifunze kutoka kwao, sio upendo wa usoni tu bali ni upendo kutoka moyoni. Yakupasa pia upende unachokifanya, ukipenda unachokifanya utakifanya kwa moyo wako. Kama bado hujapata unachokipenda jaribu kukitafuta. Hata kama mtu anakuchukia sio lazima na wewe umchukie.

Kufanya vihatarishi (Take risks), watu wengi wanaogopa kuthubutu. Wanaogopa kujaribu kufanya kitu kipya kwa kuhofu kuhusu hatari zilizopo katika kitu hicho. Wako tayari kuendelea kuwa katika hali waliyonayo badala ya kujaribu kuchukua hatua. Ni bora zaidi kufanya kitu cha kuhatarisha kuliko kukaa bila kufanya chochote.Ni hatari zaidi kukaa bila kufanya vihatarishi kuliko kufanya. Watu wengi hawajutii vile vitu ambavyo wamevifanya hata kama walishindwa bali vile ambavyo hawakufanya. Utafiti uliofanyika unaonesha kwamba wale watu wanaothubutu kufanya vitu vya hatari hushindwa mara chache zaidi kuliko kufanikiwa.

Katika vita vya pili vya dunia marubani wa ndege za kivita waliokuwa tayari kukabili hatari waliweza kuokoa maisha yao kuliko wale ambao walikuwa wakijihami zaidi na kuogopa kukabili hatari. Utafiti mwingine unaonyesha kwamba wale watu ambao huishi kwa tahadhari sana huishi muda mfupi kuliko wale wanaojiingiza katika hatari. Kufanya vitu hatarishi haimaanishi kufanya vitu vya hatari ovyo, siku zote fanya hatari ambazo umeshazipigia mahesabu, Waingereza wanasema take calculated risks.
Nakuatakia utekelezaji mwema.

Nickson Yohanes
Email: nmyohanes@gmail.com

Choma meli yako sasa

Ndugu msomaji napenda kutumia wasaa huu kuweza kukusalimia kabla sijaanza kukushirikisha niliyonayo leo. Nianze kwa kukusimulia hadithi moja:

Hapo zamani kuna kiongozi wa nchi fulani alienda vitani na jeshi lake katika nchi ya kigeni kwa kutumia usafiri wa meli. Alipofika pwani ya nchi ya adui aliamuru jeshi lake kuchoma meli waliyokwenda nayo. Aliwaambia wapiganaji wake kwamba kwa sasa wana machaguo mawili tu ambayo ni kushinda ile vita na ni lazima washinde ama kufa wote kwani hawawezi kutoka salama huko kwa kutoroka kwani wameshachoma moto meli yao. Wasiposhinda maana yake watauawa ama watakuwa mateka ama washinde vita na warudi nchini kwao salama. Hapo sasa kukawa hakuna jinsi zaidi ya jeshi lake kuwa na dhamira moja tu ya kushinda kwani kwani kwa namna yoyote hawako salama maana wakipigana wanaweza kushinda lakini pia wanaweza kufa na wasipopigana pia wanaweza kufa kwa hiyo walijitoa kwa

Hizi ndizo kanuni za kuwa na afya bora

Ili uweze kufanya shughuli zako za kila siku ikiwa ni pamoja na shughuli za uzalishaji mali ni lazima uwe na afya njema. Afya ni hali ya kuwa vizuri kimwili, kiakili, kisaikolojia na kiroho pia. Watu wengi huchukulia kuwa watu wanene ndio wenye afya njema na wakati mwingine hudhani kuwa watu wembamba ndio wenye afya. Lakini kiukweli hilo si kweli.  Mtu mwenye afya ni yule mwenye sifa nilizotaja hapo juu.

Kama huna mojawapo kati ya hivi basi hatuwezi kusema kuwa una afya njema. Ukiwa na afya njema utaweza kuishi maisha yenye furaha na amani na pia utaweza kujizalishia kipato chako kwa kila siku iendayo kwa Mungu. Ili uwe na afya njema inakupasa