Utangulizi
Maziwa ya soya ni maziwa yanayotokana na mbegu za soya. Ni kinywaji kizuri kwa afya na pia hutumika kama kiburudisho. Maziwa ya soya hufanana sana na maziwa ya wanyama hasa ya ng’ombe katika virutubisho na pia mwonekano (rangi). Maziwa ya soya ni mazuri sana kwa sababu hayana lehemu (cholesterol),mafuta yasiyofaa/mgando (saturated fats) na yana virutubisho vingi. Maziwa haya hufaa sana pia kwa watu wenye mzio (allergy) na maziwa ya wanyama kutokana na kukosa kimeng’enyo kiitwacho lactose (lactose intolerant people).
Jinsi ya kuandaa
1) Chambua soya zako kuondoa uchafu.
3) Loweka soya zako kwa muda wa saa 8 au usiku mzima ili kulainisha na pia kuondoa sumu(anti-nutritional factors).
4) Chemsha soya zako vizuri.
5) Epua na fikicha kwa vidole kuondoa maganda.
6) Ondoa maganda kwa kutumia maji ya baridi
7) Kausha soya zako na uzisage ili kupata unga.
8) Changanya kikombe kimoja cha unga wa soya na vikombe 3 vya maji.
9) Chemsha mchanganyiko wako kwa muda usiopungua dakika 30.
10) Epua na chuja mchanganyiko wako kwa kitambaa safi kuondoa makapi ya soya.
11) Ongeza sukari na viungo kama iliki, vanilla n.k.
12) Pooza maziwa yako na yatakuwa tayari kunywewa.
Njia nyingine
Fuata hatua zote mpaka hatua ya tatu.
4. Ponda ponda soya kupata uji uji mzito.
5. Chuja mchanganyo kwa kutumia kitambaa safi.
6. Chemsha mchanganyo wako kasha uuweke kwenye vyombo safi.
7. Ongeza maji kuweza kupata maziwa yako ya soya
8. Ongeza sukari na viungo kama iliki,vanilla n.k.
Email: nmyohanes@gmail.com